Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.
Halafu wabwana wa yule mujakazi wakaona kwamba hawataweza tena kupata mali kutoka kwa yule aliyekuwa kitumaini chao. Kwa hiyo wakakamata Paulo na Sila, wakawakokota na kuwapeleka mbele ya wakubwa kwenye nafasi ya makutano.
Na zaidi ya hiyo, wanashikwa na uvivu na kuwa na tabia ya kutangatanga nyumba kwa nyumba. Na si ile tu, vilevile wao ni wakatetea na wenye kujiingiza katika maneno ya watu wengine na kusema maneno yasiyofaa.