Halafu nao watajibu: ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, au kiu, au ukikuwa mugeni, au uchi, au mugonjwa, au mufungwa, nasi hatukukusaidia?’
Basi Yesu akaikaa, akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia: “Mutu anayetaka kuwa wa kwanza anapaswa kujiweka wa mwisho kuliko wote na kuwa mutumishi wa wote.”
Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”
Lakini isikuwe hivi katikati yenu. Lakini yule anayekuwa mukubwa kati yenu sherti akuwe mudogo zaidi, na yule anayekuwa mwongozi sherti akuwe kama mutumishi.
Yesu akajibu: “Ufalme wangu si wa dunia hii. Ufalme wangu ungekuwa wa dunia hii, watumishi wangu wangenipigania kusudi nisitolewe kwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa katika dunia.”
Nao walipofika katika muji Salami, wakahubiri Neno la Mungu katika nyumba za kuabudia za Wayuda. Yoane alikuwa pamoja nao, akiwasaidia kwa kufanya kazi.
Hatutafuti kuwaamuru ninyi juu ya mambo yale munayopaswa kuamini, maana munasimama imara katika imani. Lakini tunataka kutumika pamoja nanyi kusudi mupate kufurahi.
Yule anayehubiri, anapaswa kutoa ujumbe wa Mungu. Na yule anayetumika, atumike kwa kadiri ya nguvu alizopewa na Mungu, kusudi Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo anayekuwa mwenye utukufu na uwezo kwa milele na milele. Amina.
Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.