Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 20:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Yesu akamwuliza: “Unataka nini?” Naye akamujibu: “Utakapokuwa katika Ufalme wako, uwaruhusu hawa wana wangu wawili kuikaa, mumoja kwa upande wako wa kuume na mwingine kwa upande wako wa kushoto.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 20:21
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Batiseba akamwendea mufalme Solomono kwa kumwelezea ombi la Adonia. Mufalme akasimama kwenda kumupokea mama yake, akainama mbele yake. Halafu, akaikaa katika kiti chake cha kifalme, akaagiza mama yake aletewe kiti, naye akaikaa kwa upande wa kuume wa mufalme.


Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”


Hapo mufalme akauliza: “Unataka nini Esteri? Uniambie unachotaka, nawe utapata – hata kama ni nusu ya ufalme wangu.”


Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


Nguo zako zinanuka marasi, udi, na mudalasini; muziki wa vinubi unakufurahisha katika nyumba ya pembe za tembo.


Wewe unajitakia wewe mwenyewe mambo makubwamakubwa? Usiyatafute! Achana nayo, maana ninaleta maangamizi juu ya wanadamu wote. Pato lako ni hili: nitayaokoa maisha yako kila nafasi utakapokwenda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wakati ule wanafunzi wakamufikia Yesu, wakamwuliza: “Ni nani anayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni?”


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.


Yesu akawaambia: “Hamujui kitu munachoomba. Munaweza kubeba muzigo wa mateso nitakaoubeba?” Nao wakamujibu: “Tunaweza.”


Yesu akasimama na kuwaita. Akawauliza: “Munataka niwafanyie nini?”


Yesu akamwuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akamujibu: “Mwalimu, ninataka nipate kuona.”


Bwana Yesu alipokwisha kusema nao maneno hayo, akanyanyuliwa juu kwenda mbinguni na kuikaa kwa upande wa kuume wa Mungu.


Binti ya Herodia aliingia na kucheza hata Herode na waalikwa wake wakapendezwa. Halafu mufalme akamwambia yule binti: “Uniombe kitu chochote unachotaka, nami nitakupa.”


“Unataka nikufanyie nini?” Akamujibu: “Bwana, ninataka nipate kuona.”


Watu walipokuwa wakisikiliza maneno hayo, Yesu akaongeza kuwaambia mufano mumoja, kwa sababu alikuwa karibu na muji Yerusalema, na watu wale walizani kwamba siku za Ufalme wa Mungu zitafika saa ile ile.


Kulitokea ubishi kati ya wanafunzi wa kujua nani anayekuwa mukubwa kati yao.


Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


Basi mitume walipokusanyika pamoja na Yesu, wakamwuliza: “Bwana, wakati huu ndio utakapowarudishia Waisraeli ufalme wao?”


Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.


Ni nani anayeweza basi kuwahukumu? Hakuna hata mumoja! Maana Yesu Kristo ndiye aliyekufa, na zaidi ya hiyo, alifufuka, na sasa anakaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, na yeye ndiye anayetuombea.


Kwa kuwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, mutafute mambo yanayokuwa juu, pahali Kristo anapoikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ