9 Kisha kumusikiliza mufalme, wakaondoka. Ile nyota waliyoiona tokea mashariki iliwatangulia, nayo ikaenda na kusimama juu ya pahali mutoto alipokuwa.
Kila mutu anayemwabudu Yawe, Yawe atamufundisha njia ya kufuata.
Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.
Na wakati walipoiona wakafurahi sana.
Nao wakauliza: “Yuko wapi yule mutoto aliyezaliwa kuwa mufalme wa Wayuda? Tumeona nyota yake inayomutambulisha, nasi tumekuja kumwabudu.”
Kisha akawatuma Betelehemu, akiwaambia: “Mwende mupeleleze habari kamili za mutoto yule. Nanyi mutakapomwona munijulishe kusudi mimi vilevile niende kumwabudu.”
Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.