waliwasimamia wabebaji wa mizigo na kuwaongoza wote waliofanya kazi mbalimbali, na kati ya Walawi kulikuwa waandishi, wakubwa na hata walinzi wa mulango.
Hata makuhani, viongozi wa inchi ya Yuda pamoja na watu walikosa uaminifu kabisa wakiiga matendo yote ya kuchukiza ya watu wa mataifa mengine; waliichafua nyumba ya Yawe ambayo yeye mwenyewe alikuwa ameitakasa kule Yerusalema.
Ezra akasimama na kuanza kuwaapiza makuhani, viongozi, Walawi na Waisraeli wengine wote kwamba watafanya kama ilivyosemwa, nao wakakubali kufanya kiapo.
Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.
Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.
Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”
Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakachukizwa kwa kuona miujiza aliyoifanya na watoto waliokuwa wakilalamika katika hekalu, wakisema: “Usifiwe wewe, mwana wa Daudi!”
Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”
Yesu alipokuwa hajamaliza kusema, Yuda, mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, akafika pamoja na kundi kubwa la watu wenye panga na magongo. Hawa wote walikuwa wametumwa na wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu.
Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”
Yuda akatwaa kundi la waaskari pamoja na walinzi waliotumwa na wakubwa wa makuhani na Wafarisayo. Akakuja nao kwenye bustani wakibeba taa, mienge na silaha.
Basi kukakuwa makelele mengi, na walimu wamoja wa Sheria waliokuwa wa chama cha Wafarisayo wakasimama na kubishana kwa nguvu, wakisema: “Hatuoni ubaya wowote juu ya mutu huyu. Labda roho au malaika wamesema naye!”