Mufalme wa Aramu akafazaishwa sana na hali hiyo. Akawaita wakubwa wa waaskari wake, akawauliza: “Muniambie ni nani kati yenu anayekuwa upande wa mufalme wa Israeli?”
“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!
Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”
Wao walichukizwa sana kwa sababu wale mitume wawili walikuwa wakiwafundisha watu na kutangaza kwao kwamba Yesu alifufuka, nao ufufuko wake unahakikisha kwamba wafu watafufuka.