Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 2:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Lakini aliposikia kwamba Arkelao alitawala katika jimbo la Yudea kwa pahali pa baba yake Herode, Yosefu akaogopa kwenda kule. Na alipokwisha kuonywa katika ndoto, akaenda katika jimbo la Galilaya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 2:22
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe atakulinda katika shuguli zako zote tangu sasa na hata milele.


Muangalie kuta zake na kuchunguza pango zake za kukimbilia, mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:


Wewe unaniongoza kwa mashauri yako; na kwa mwisho utanipokea kwenye utukufu.


Mukienda kwa upande wa kuume au kushoto, mutasikia sauti nyuma yenu ikisema: Njia ni hii; muifuate.


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Yesu alizaliwa Betelehemu katika Yudea wakati wa utawala wa mufalme Herode. Kisha kuzaliwa kwake, watu wenye elimu kutoka mashariki wakafika Yerusalema.


Herode alipokuwa amekwisha kufa, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto kule Misri.


Basi Yosefu akaamuka, akamutwaa mutoto pamoja na mama yake na kurudia katika inchi ya Israeli.


Wakati ule Yesu akatoka Galilaya na kufika kwenye muto Yordani, akamwendea Yoane kusudi abatizwe naye.


Wakati wazazi wa Yesu walipokwisha kutimiza kanuni zote zilizoagizwa na Sheria ya Bwana, wakarudia pamoja naye Galilaya, katika muji wao wa Nazareti.


Wakamujibu: “Na wewe vilevile umetoka Galilaya? Uchunguze Maandiko Matakatifu, nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki nabii.” [


Samweli akasema: “Nitaweza kwenda namna gani? Kama Saulo akisikia habari hiyo, ataniua!” Yawe akamwambia: “Twaa mwana-ngombe pamoja nawe, na ukifika kule useme: ‘Nimekuja kumutolea Yawe sadaka’.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ