Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu alizaliwa Betelehemu katika Yudea wakati wa utawala wa mufalme Herode. Kisha kuzaliwa kwake, watu wenye elimu kutoka mashariki wakafika Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 2:1
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Inchi walimokaa ilienea toka Mesa mpaka Sefari katika inchi ya vilima vya upande wa mashariki.


Lakini akawapa wana wa habara zake zawadi. Na wakati alipokuwa bado muzima, akawapeleka katika inchi ya upande wa mashariki, mbali na mwana wake Isaka.


Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu, na Harefu, mwanzilishi wa muji wa Beti-Gaderi.


Alikuwa na mali, kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, ngombe elfu moja, punda dike mia tano, na watumishi wengi sana. Yeye alikuwa wa heshima kuliko watu wote kule upande wa mashariki.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Lakini hakulala naye mpaka alipozaa yule mutoto mwanaume. Yosefu akamwita jina lake Yesu.


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Herode alipokuwa amekwisha kufa, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto kule Misri.


Mufalme Herode aliposikia maneno haya, akafazaika sana pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema.


Nao wakamujibu: “Betelehemu katika Yudea, kwa maana ilisemwa hivi kwa njia ya nabii:


Basi Herode akawaita kwa siri wale wenye elimu kusudi wamujulishe hakika wakati gani nyota ile ilipotokea.


Katika siku Herode alipokuwa mufalme wa Yudea, kulikuwa kuhani mumoja, aliyeitwa Zakaria, wa kundi la makuhani wa ukoo wa Abiya. Muke wake Elizabeti alikuwa vilevile wa uzao wa Kuhani Mukubwa Haruni.


Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.


Wale wamalaika walipoondoka na kurudia mbinguni, wachungaji wakasemezana: “Basi tuende Betelehemu, kusudi tupate kuona jambo lile lililotokea, ambalo Bwana alitujulisha.”


Maandiko Matakatifu hayakusema kwamba Kristo atazaliwa katika ukoo wa mufalme Daudi na katika muji Betelehemu, pahali Daudi alipoishi?”


Wakati ule kulikuwa kijana mumoja Mulawi katika muji wa Betelehemu katika inchi ya Yuda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ