Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 19:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Hivi wao si wawili tena, lakini wanakuwa mumoja. Basi mutu asitenganishe kile Mungu alichokiunganisha.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 19:6
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

mwanamuke anayemwacha mwenzake wa ujana wake, na kusahau agano la Mungu wake.


Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninachukia kuachana. Ninachukia wakati mumoja wenu anapomutendea muke wake ubaya ule. Muhakikishe kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


na kisha akasema: ‘Kwa sababu hii, mutu atawaacha baba yake na mama yake na kuungana na muke wake, nao wawili watakuwa mwili mumoja.’


Halafu Wafarisayo wakamwuliza: “Kwa sababu gani basi Musa aliamuru kuandika barua ya kuachana wakati wa kumufukuza mwanamuke?”


Basi mutu asitenganishe kile Mungu alichokiunganisha.”


Kwa mufano, mwanamuke aliyeolewa anafungwa na Sheria katika maisha yake na mume wake wakati mume wake angali muzima. Lakini kama mume wake akikufa, yeye anakuwa huru kufuatana na Sheria ile iliyomufunga.


Hivi vilevile waume wanapaswa kupenda wake wao kama vile wanavyopenda miili yao wenyewe. Yule anayependa muke wake, anajipenda yeye mwenyewe.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ