Ninasikitika kwa ajili yako, ndugu yangu Yonatani. Umekuwa kwangu mutu wa kupendeza siku zote. Pendo lako kwangu limekuwa la ajabu, la ajabu kuliko la mwanamuke.
ni kusema wanawake wa mataifa ambayo Yawe alikuwa amewakataza Waisraeli akisema: “Musioe kwao wala wao wasioe kwenu kwa sababu wanawake hao watapotosha mioyo yenu kusudi muitumikie miungu yao.” Solomono aliwapenda sana wanawake hao.
Mungu hakuwafanya ninyi wote wawili mukuwe mwili mumoja na roho moja? Alikusudia nini alipofanya hayo? Tuzae watoto wanaomupendeza Mungu. Kwa hiyo, muchunge uzima wenu na kuhakikisha kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.
Au hamujui kwamba mutu yule anayeungana na kahaba amekwisha kuwa mwili mumoja naye? Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Hao wawili watakuwa mwili mumoja.”
Muke hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa mume wake. Vilevile mume hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa muke wake.
Ni sawasawa inavyosemwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu hii, mume ataacha baba yake na mama yake na kuungana na muke wake, nao wawili watakuwa mwili mumoja.”
Saulo alipomaliza kuzungumuza na Daudi, Yonatani mwana wa Saulo alivutwa sana na Daudi, akamupenda kwa moyo wake wote kama alivyojipenda yeye mwenyewe.