Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 19:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 uwaheshimu baba yako na mama yako na kumupenda mwenzako sawa wewe mwenyewe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 19:19
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Kama mutu akimuchekelea baba yake na kuzarau utii kwa mama yake, macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori na kuliwa na tai.


Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.


Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Yule kijana akamwambia: “Nimetii hizo amri zote. Ninakosewa na nini tena?”


Na ya pili inayofanana nayo ni hii: ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’


“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Umupende mwenzako, lakini umuchukie adui yako.’


Mutu yule akamujibu kwa maneno haya: “ ‘Umupende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu yako yote na kwa akili yako yote.’ Vilevile, ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’ ”


Kwa hiyo amri hizi: “Usizini, usiue, usiibe, usitamani,” pamoja na zingine zote, zinafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako sawa vile unavyojipenda mwenyewe.”


Kwa maana Sheria yote inafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.”


“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ