Mutu yule akamujibu kwa maneno haya: “ ‘Umupende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu yako yote na kwa akili yako yote.’ Vilevile, ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’ ”
Kwa hiyo amri hizi: “Usizini, usiue, usiibe, usitamani,” pamoja na zingine zote, zinafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako sawa vile unavyojipenda mwenyewe.”
“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.