Kulingana na hayo, watu wamoja hawawezi kuoa kwa sababu walizaliwa towashi, wengine wamefanywa kuwa towashi na watu, wengine wamejifanya vile wenyewe kwa sababu ya kutumikia Ufalme wa mbinguni. Anayeweza kukubali mafundisho haya, ayakubali!”
Kwa ngambo ingine, kila mutu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote.
Maneno hayo ninayosema ni kwa faida yenu, wala si kwa kuwafungia njia. Ninataka kuwaonyesha namna ya kuishi sawa inavyofaa, kusudi mupate kumutumikia Bwana pasipo kizuizo chochote.