Huyo musimamizi akasema: “Sawa. Ikuwe kama mulivyosema. Yeyote atakayepatikana na kikombe hicho, atakuwa mutumwa wangu, lakini wengine wote hamutakuwa na kosa.”
walitoa kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu: toni mia moja makumi saba za zahabu, vikoroti elfu kumi vya zahabu, na zaidi ya toni mia tatu za feza, yapata toni mia sita za shaba, na zaidi ya toni elfu mia tatu za chuma.
nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.
Na kwa kuona mutumishi yule hakukuwa na jinsi ya kulipa deni lile, bwana wake akaamuru auzishwe kuwa mutumwa, yeye na muke wake pamoja na watoto wake na vyote alivyokuwa navyo viuzishwe vilevile, kusudi apate kumulipa.
Yule mutumishi aliyepewa furushi tano za zahabu, akakuja, akaleta faida ya zingine tano. Na akasema: ‘Bwana, umenipatia furushi tano za zahabu, na sasa angalia, kuna faida ya zingine tano.’
Kisha yule mutumishi aliyepewa furushi moja akakuja, akasema: ‘Bwana, nilijua kuwa wewe ni mutu mugumu anayevuna nafasi asipopanda, na kukusanya nafasi asiposambaza.
Vilevile munazani kwamba wale watu kumi na wanane waliokufa munara ulipowaangukia kule Siloamu, walikuwa wakosaji kuliko wakaaji wengine wote wa Yerusalema?
Kisha akamwuliza mwingine: ‘Na wewe uko na deni yapata gani?’ Naye akajibu: ‘Saki mia moja za ngano.’ Yule mulinzi akamwambia: ‘Kamata barua yako ya mapatano na uandike saki makumi nane.’