Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 18:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 “Kweli ninawaambia tena: wawili kati yenu hapa katika dunia wakipatana kwa kuomba juu ya kitu chochote, Baba yangu anayekuwa mbinguni atawapa kitu kile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 18:19
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


uache sadaka yako pale mbele ya mazabahu na uende kwanza kusikilizana naye. Na kisha urudie na kutoa sadaka yako.


“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.


Ni kwa hiyo ninawaambia kwamba munapoomba kwa ajili ya hitaji la kitu fulani, mwamini kama mumekwisha kukipokea, na kwa njia hiyo mutakipewa.


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


“Siku ile itakapotimia, ninyi hamutaniuliza juu ya kitu fulani. Kweli, kweli ninawaambia: Baba atawapa chochote mutakachomwomba kwa jina langu.


Hawa wote walikuwa wakikusanyika kwa nia moja kwa kuomba, pamoja na wanawake wamoja, Maria mama wa Yesu, na wandugu za Yesu.


Basi Petro akabaki akichungwa katika kifungo, lakini kanisa likaendelea kumwombea kwa Mungu pasipo kuchoka.


Na pale pale kisha kupata maono yale, tukajitayarisha kwenda Makedonia, kwa maana tulitambua hakika kwamba Mungu alituita kwenda kuhubiri Habari Njema kule.


Na sisi kwa ngambo yetu tutajitolea kwa kuomba Mungu na kuhubiri neno lake.”


kwa maana ninajua kwamba kwa ajili ya maombi yenu na kwa musaada wa Roho wa Yesu Kristo nitakombolewa.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ