Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 18:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 “Munafikiri nini? Kama mutu akiwa na kondoo mia moja, na mumoja wao akipotea, hatawaacha wale wengine makumi tisa na tisa juu ya mulima na kwenda kumutafuta yule aliyepotea?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 18:12
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, neno la Yawe lilimufikia Elia wa Tisibe kusema hivi:


Ninatangatanga kama kondoo aliyepotea; ukuje kunitafuta mimi mutumishi wako, maana sikusahau amri zako.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Watu wangu walikuwa kama kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea kwenye milima; walitembea toka mulima mpaka kilima, wakasahau makao yao.


Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.


Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


Hawatakamatwa tena mateka na mataifa mengine wala nyama wa pori hawatawaua na kuwakula. Wataishi kwa usalama na hakuna atakayewatisha.


Wanaokuwa zaifu hamukuwatia nguvu, wagonjwa hamukuwatunza, waliovunjika hamukuwafunga kwa kitambaa, waliotangatanga hamukuwarudisha na waliopotea hamukuwatafuta. Lakini mukawatawala kwa kinguvu na kuwatesa.


Kweli, kondoo walisambazwa, wakatangatanga juu ya milima na vilima. Kondoo walisambazwa katika dunia yote, na hakukukuwa mutu aliyejali juu yao wala kuwatafuta.


Yesu akawajibu: “Kama mutu mumoja kati yenu akiwa na kondoo mumoja, na kondoo yule akitumbukia ndani ya shimo kwa siku ya Sabato, hatamukamata na kumwondosha mule siku ile ile?


Na kama akimupata yule kondoo, kweli ninawaambia, anamufurahia kuliko wale makumi tisa na tisa waliobaki bila kupotea.


Yesu akaongeza kusema: “Ninyi munafikiri nini juu ya habari hii? Kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa na watoto wawili. Yeye akamwambia mutoto wa kwanza: ‘Mutoto wangu, ninataka uende leo kutumika katika shamba langu la mizabibu.’


“Munafikiri nini juu ya Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Nao wakamujibu: “Yeye ni mwana wa Daudi.”


Ninasema nanyi kama watu wenye akili; muamue ninyi wenyewe juu ya maneno ninayotaka kuwaambia:


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ