Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 17:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wanafunzi wale waliposikia sauti ile, wakaogopa sana, wakaanguka uso mpaka chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 17:6
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.


Basi, nikasimama na kwenda katika bonde. Nikiwa huko nikauona utukufu wa Yawe ukiwa umesimama huko kama utukufu ule niliokuwa nimeuona karibu na muto Kebari; nami nikaanguka uso mpaka chini.


Maono hayo yalikuwa kama maono niliyoyaona wakati Mungu alipokuja kuuangamiza Yerusalema. Vilevile yalifanana na maono niliyoyaona karibu na muto Kebari. Nikaanguka uso mpaka chini.


Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Lakini Yesu akawajongelea, akawagusa na kuwaambia: “Musimame, musiogope.”


Nikaanguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa?’


Sisi wote tukaanguka chini, na nikasikia sauti iliyoniambia hivi katika luga ya Kiebrania: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa? Unajiumiza bure kama ngombe anayepiga teke kwenye chongo ya fimbo ya mwenyeji wake.’


Sisi wenyewe tuliisikia sauti ile toka mbinguni tulipokuwa pamoja naye juu ya mulima mutakatifu.


Basi wakati Manoa na muke wake walipokuwa wanaangalia ndimi za moto zikipanda juu mbinguni kutoka kwenye mazabahu, wakamwona malaika katika ndimi hizo akipanda kwenda mbinguni. Basi Manoa na muke wake wakainama uso mpaka chini.


Basi, Manoa akamwambia muke wake: “Hakika tutakufa, maana tumemwona Mungu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ