Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 17:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 17:5
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akamujibu Yobu kutoka katika zoruba:


“Mimi nilikutua mizigo yako toka kwenye mabega, nilikuondolea matofali uliyochukua katika mikono.


Sauti ya baragumu ikazidi kuongezeka na Musa akaongea na Mungu. Mungu naye akamujibu katika ngurumo.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Kwa ajili ya uaminifu wake, Yawe, alipenda kutukuza sheria yake na kuiheshimisha.


“Muangalie, mutumishi wangu niliyejichagulia, anayekuwa mupendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitamujaza Roho wangu, naye atatangaza haki yangu kwa mataifa.


Wanafunzi wale waliposikia sauti ile, wakaogopa sana, wakaanguka uso mpaka chini.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”


Halafu wingu likatokea na kuwafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa. Mumusikilize!”


na Roho Mutakatifu akashuka juu yake katika hali ya kimwili kwa mufano wa njiwa. Na sauti ikasikilika toka mbinguni ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


Na Baba aliyenituma amenishuhudia vilevile. Ninyi hamujasikia sauti yake wakati wowote wala hamujaona sura yake.


Kisha kusema maneno haya, Yesu akanyanyuliwa mbinguni, nao walikuwa wakimwangalia. Na wingu likamuficha hata hawakumwona tena.


Ni yule yule Musa ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: ‘Mungu atawatumia ninyi nabii anayekuwa sawa mimi, toka katika taifa lenu.’


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Yeyote ambaye hatasikia maneno nabii huyo atakayosema kwa jina langu, mimi mwenyewe nitamwazibu.


“Hizi ndizo amri Yawe alizowaambia ninyi wote kwa sauti kubwa kutoka katika moto na lile wingu zito na giza nene, mulipokuwa mumekusanyika kule kwenye mulima. Hakuongeza hapo amri ingine. Kisha akaandika juu ya vibao viwili vya mawe, akanipatia.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


Niliangalia tena, nami nikaona wingu jeupe, na juu ya wingu lile kulikuwa kukiikaa kiumbe kimoja kinachofanana na Mwana wa Mutu. Juu ya kichwa chake kulikuwa taji la zahabu, naye alikuwa akishika kisu kikali cha kuvuna katika mukono wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ