“Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia.
Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.
Kisha nikaona malaika mwingine mwenye uwezo akishuka toka mbinguni. Alikuwa akifunikwa na wingu, naye alikuwa na upindi wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingaa kama jua na miguu yake ilimetameta kama nguzo ya ndimi za moto.