Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 17:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Yesu akamukaripia yule pepo aliyekuwa ndani ya yule mutoto, naye akamwacha, na tangia saa ile ile yule mutoto akapona.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 17:18
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wakamuletea Yesu mutu mumoja aliyeshikwa na pepo, aliyemufanya kuwa kipofu na bubu. Yesu akamuponyesha mutu yule hata akaanza kusema na kuona.


Halafu Yesu akamujibu: “Wewe mwanamuke, imani yako ni kubwa! Ifanyike kwako sawa ulivyoomba.” Na binti yake akapona tangia saa ile ile.


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Kisha wanafunzi wakamufikia Yesu, wakiwa peke yao, na kumwuliza: “Kwa nini sisi hatukuweza kumufukuza yule pepo?”


Naye Yesu alipogeuka, akamwona na kumwambia: “Binti yangu, ujipe moyo! Imani yako imekuponyesha.” Na mwanamuke yule akapona saa ile ile.


Yesu akawaponyesha watu wengi wenye magonjwa mbalimbali. Vilevile alifukuza pepo wengi, wala hakuwaachilia pepo kusema neno, kwa sababu walimujua yeye ni nani.


(Alisema hivi kwa sababu Yesu alikuwa akimwamuru: “Wewe pepo, toka ndani ya mutu huyu!”)


Pepo wakatoka ndani ya watu wengi, wakilalamika, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakaripia, na hakuwaachilia waseme neno, kwa sababu walijua kwamba yeye ndiye Kristo.


Alisema vile kwa sababu Yesu alikuwa amemwamuru huyo pepo, atoke ndani ya yule mutu. Huyo pepo alimukamata mutu yule mara nyingi, na ijapokuwa watu walimufunga na minyororo na vifungo vya chuma kusudi asitoroke, yeye alivikata. Na yule pepo alimusukuma kwenda katika jangwa.


Yule mutoto alipokuwa akijongea karibu na Yesu, yule pepo akamutupa chini na kumutikisa kwa nguvu. Lakini Yesu akamukaripia yule pepo na kumuponyesha mutoto. Kisha akamurudisha kwa baba yake.


Naye akafanya hivi kwa muda wa siku nyingi. Na kwa mwisho Paulo akachukizwa naye. Basi akageuka na kumwambia yule pepo: “Ninakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, utoke ndani yake!” Na saa ile ile yule pepo akatoka ndani yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ