Matayo 17:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Lakini ninawaambia kama Elia amekwisha kurudi, nao hawakumutambua, lakini walimutendea yote waliyotaka. Ni vile ndivyo Mwana wa Mutu atateswa nao vilevile.”
Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.
Kwa maana Yoane alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, nanyi hamukumusadiki. Lakini walipishaji wa kodi na makahaba walimusadiki. Na ijapokuwa muliona mambo hayo yote, hamukugeuka toka zambi zenu na kumusadiki.”
Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.
Kwa hiyo, ninyi wote pamoja na Waisraeli wote mujue vizuri kwamba mutu huyu anayesimama mbele yenu akiwa muzima kabisa, ni kwa uwezo wa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, yule muliyemutundika juu ya musalaba, lakini Mungu amemufufua.
Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.