Wakati ule, yule mutumishi aliyetumwa kwenda kwa Mikaya, akamwambia: “Manabii wengine wote kwa pamoja, wamemutabiria mufalme ushindi. Tafazali, nawe vilevile ufanye kama wao, umutabirie mazuri.”
Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.
Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”