Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 15:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ibada wanayonifanyia ni ya bure, sababu mafundisho yao yanalingana na kanuni za watu tu.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 15:9
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Kweli ni kwa bure nimejichunga katika usafi wa moyo, na kujilinda nisitende zambi?


Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


basi, mimi nitafanya hivi: Nitawapiga kwa kuwaletea hofu kubwa ya rafla, kifua kikubwa na homa itakayowapofusha macho na kuwakondesha. Mutapanda mbegu zenu bila mafanikio maana waadui zenu ndio watakaozikula.


Mutatumia nguvu zenu bure maana mashamba yenu hayatatoa mavuno na inchi yenu haitazaa matunda.


Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza?


Kisha Yesu akaita kundi la watu na kuwaambia: “Musikilize na kuelewa maneno nitakayowaambia.


Ibada wanayonifanyia ni ya bure, sababu mafundisho yao yanalingana na kanuni za watu tu.’ ”


Nanyi kwa njia ya habari hiyo munaokolewa, ikiwa munaishika kufuatana na maneno niliyowahubiri. Kama isipokuwa hivi, muliamini bure.


Uwaambie wasishikamane na hadisi za uongo, pamoja na mambo yasiyokuwa na mwisho ya wababu. Hayo yote yanaleta mabishano, wala hayafai kitu kwa kutimiza mupango wa Mungu wa wokovu, unaojulikana kwa njia ya imani.


Na zaidi ya ile hawatafuata hadisi za uongo za Kiyuda wala maagizo ya watu waliopotoka mbali na ukweli.


Musidanganywe na mafundisho mengine ya kigeni ya kila namna. Kwa maana mioyo yetu inapaswa kutiwa nguvu kwa njia ya neema ya Mungu, wala si kwa njia ya kushika kanuni zinazoagizwa juu ya vyakula. Kanuni hizo haziwafalii kitu wale wanaozishika.


Wewe mujinga! Unataka kuhakikishwa kwamba imani pasipo matendo ni bure?


Mimi Yoane ninatoa maonyo haya kwa kila mutu anayesikia maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki: kama mutu akiongeza kitu juu ya maneno haya, Mungu atamwongezea mapigo yale yanayoandikwa katika kitabu hiki.


Daudi alikuwa akifikiri: “Mimi nimekuwa nikilinda mali yote ya Nabali katika jangwa bila faida yoyote na hakuna kitu chake chochote kilichopotea, naye amenilipa mabaya kwa mazuri niliyomutendea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ