Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 15:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Yale makundi ya watu wakashangaa sana wakati walipowaona wabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanatembea, na vipofu wanaona. Nao wakamusifu Mungu wa Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 15:31
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Basi, akajenga mazabahu pahali pale na kuiita “Mungu ni Mungu wa Israeli”.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Anayenitolea shukrani kama sadaka yake, huyo ndiye anayenitukuza; yeyote anayedumu katika njia yangu, huyo ndiye nitakayemwokoa.”


wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, kikiwa safi kama mbingu inayoangaa.


Halafu makundi mengi ya watu wakamufikia, wakimuletea vilema, vipofu, viwete na wabubu. Wakawaweka mbele ya Yesu, naye akawaponyesha.


“Kama mukono wako au muguu wako ukikukosesha, uukate na kuutupa mbali! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukikuwa na mukono mumoja au ukikuwa kilema. Hiyo ni vizuri kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili na kutupwa katika moto kwa milele.


Vipofu na viwete wakamufikia Yesu kule ndani ya hekalu, naye akawaponyesha.


Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa na kuwaambia watu waliomufuata: “Kweli ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli, sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.


Watu hao wawili walipokwisha kwenda, wakamuletea Yesu mutu mumoja bubu aliyeshikwa na pepo.


Wakati Yesu alipokwisha kumufukuza yule pepo, yule bubu akaanza kusema. Nao watu wote wakashangaa na kusema: “Hatujaona jambo kama hili katika inchi yote ya Israeli!”


Watu walipoona jambo hilo wakaogopa na kumusifu Mungu aliyewapa watu mamlaka ya namna ile.


Na watu wote walipokuwa wakimwangalia mutu yule, pale pale akasimama, akatwaa kipoyi chake na kujiendea. Wote wakashangaa, wakamusifu Mungu, wakisema: “Hatujaona mambo kama haya hata mara moja!”


Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”


Kama mukono wako ukikukosesha, uukate! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukiwa na mukono mumoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika jehenamu ndani ya moto usiozimika. [


Lakini wakati unapofanya karamu, uwaalike wamasikini, vilema, viwete na vipofu.


Basi yule mutumishi akarudia na kumwelezea bwana wake maneno hayo yote. Halafu bwana wa nyumba akakasirika, na kumwambia: ‘Kwenda upesi katika nafasi za mukutano na katika barabara za muji, uwalete wamasikini, vilema, vipofu na viwete na kuwaingiza humu.’


Na pale pale akapata kuona, na kumufuata Yesu akishukuru Mungu. Na watu wote walipoona jambo hili wakamusifu Mungu.


Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ