ndilo taifa la Waisraeli. Wao walikubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, yeye aliwaonyesha utukufu, alifanya maagano nao, aliwapa Sheria, aliwaonyesha namna ya kumwabudu na kuwatolea ahadi zake.
Kwa wakati ule mulikuwa mumetengwa mbali na Kristo. Hamukukuwa kati ya watu waliochaguliwa na Mungu, mulikuwa wageni kati yao. Ninyi hamukukuwa na pato lolote katika agano zile Mungu alizotoa katika ahadi yake kwa watu wake. Muliishi katika dunia pasipo tumaini wala kumujua Mungu.