Ilipotimia siku ya tatu, ambayo ilikuwa siku ya kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake, mufalme wa Misri akafanyia watumishi wake wote karamu. Akatoa katika kifungo mutunza vinywaji wake mukubwa na mupishi mukubwa wa mikate, akawaweka mbele ya wakubwa wake.
Kisha mufalme akafanya karamu kubwa kwa heshima ya Esteri, akawaalika viongozi na watumishi wote wa serikali yake. Vilevile, mufalme akatangaza musamaha wa kodi katika majimbo yote, akatoa zawadi nyingi kulingana na mapato yake ya kifalme.
Herode alikuwa amemukamata Yoane akamufunga minyororo na kumutia ndani ya kifungo. Herode alifanya vile kwa sababu ya Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.
Mufalme Herode alisikia habari za Yesu, kwa maana jina lake lilikuwa limevuma fasi zote. Watu wamoja walisema: “Huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”
Ni Herode mwenyewe aliyeamuru kwamba Yoane akamatwe na kutiwa katika kifungo. Ilitokea vile kwa sababu Herode alimwoa Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,
na Yoana muke wa Kuza, huyo mume wake alikuwa musimamizi wa mali ya Herode, pamoja na Suzana na wengine wengi. Wanawake hawa walitumia mali yao kwa kuwasaidia Yesu na wanafunzi wake.
“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.