30 Lakini alipoona upepo, akaogopa, na kwa vile alivyoanza kuzama ndani ya maji, akalalamika akisema: “Bwana, uniokoe!”
Mutumishi wa Elisha alipoamuka mapema kesho yake na kutoka inje, akaona waaskari pamoja na farasi na magari ya vita wameuzunguka muji. Akarudi ndani akasema: “Ole wetu, ee, Bwana wangu! Sasa tutafanya nini?”
Sitaogopa maelfu ya watu wanaonizunguka kila upande.
Naye Yesu akamujibu: “Kuja.” Halafu Petro akatoka ndani ya chombo, akaanza kutembea juu ya maji kumufikia Yesu.
Mara moja Yesu akanyoosha mukono, akamushika na kumwambia: “Ee wewe mwenye imani ndogo! Kwa sababu gani uliona shaka?”
Mukeshe na kuomba, kusudi musianguke katika majaribu; kwa maana roho ni hodari, lakini mwili ni zaifu.”