Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu. [
Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: mukimwamini Mungu pasipo kuwa na shaka, hamutaweza kufanya tu kama nilivyotendea muti huu, lakini vilevile mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Ondoka hapa, ujitupe katika bahari,’ na itakuwa vile.
Bwana akajibu: “Kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya haradali, mutaweza kuuambia muti huu wa mukuyu: ‘Ujiongoe hapa na uende kujipanda katika bahari,’ nao ungewatii.
Mutu huyu munayemujua na kumwona amepata tena nguvu kwa uwezo wa jina la Yesu, kwa njia ya kuaminia jina hili. Yeye amepona kabisa sawa vile ninyi wote munavyojionea, kwa njia ya kumwaminia Yesu.
Yeye alikuwa na umri wa miaka karibu mia moja, lakini imani yake haikupunguka alipofikiri juu ya hali yake iliyokuwa kama ya mwenye kungojea tu lufu wala juu ya hali ya Sara aliyekuwa hawezi tena kuzaa.