Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 14:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Kisha kuwaamuru watu waikae juu ya majani, Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakaigawanya kwa kundi la watu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 14:19
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi Yesu akawaamuru wanafunzi wake wawaambie watu wote waikae chini kwenye majani kwa makundi mbalimbali.


Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake pamoja na zile samaki mbili kusudi waigawanyie watu wote.


Kisha Yesu akaangalia juu mbinguni, akasisimua na kumwambia yule mutu: “Efata,” maana yake, “Funguka!”


Kisha Yesu akatwaa kikombe, akakibariki na kusema: “Mutwae kikombe hiki na mukigawanye kati yenu.


Halafu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa akisema: “Huu ni mwili wangu [unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.


(Watu waliokuwa pale walikuwa yapata wanaume elfu tano.) Yesu akawaamuru wanafunzi wake wawaikalishe kwa makundi ya watu makumi tano tano.


Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Halafu akaimega, akawapa wanafunzi waigawanyie watu.


Basi wakaondosha lile jiwe. Yesu akainua macho juu, akasema: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia.


Na vilevile vyombo vingine vilivyotoka katika muji Tiberia vilifika karibu na pahali pale walipokula mikate, Bwana alipokuwa amekwisha kushukuru Mungu.


Kisha kusema maneno hayo, Paulo akatwaa mukate, akamushukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, na akaanza kula.


Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.


tunapokunywa kikombe ambacho kwa ajili yake tunamutolea Mungu shukrani, basi kwa njia ya kikombe kile hatuungani na damu ya Kristo? Nasi tunapomega mukate na kuukula, kwa njia hiyo, mukate ule hautuungi na mwili wa Kristo?


Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


na alipokwisha kumushukuru Mungu, akaumega akisema: “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ