Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 13:47 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

47 “Ufalme wa mbinguni unafanana vilevile na wavuvi wamoja waliotupa wavu ndani ya ziwa, nao ukakusanya samaki wa kila namna.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 13:47
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wavuvi watasimama kandokando ya bahari, na nafasi toka Engedi mpaka Eni-Eglaimu itakuwa ya kuanikia nyavu. Kutakuwa aina nyingi za samaki kama zinavyokuwa katika bahari ya Mediteranea.


“Ufalme wa mbinguni unafanana na mali iliyofichwa katika shamba moja. Mutu mumoja alipoiona, akaificha tena. Halafu kwa furaha kubwa akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kununua lile shamba.


Alipoona ushanga mumoja muzuri sana, akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kuununua.


Wakati wavu ulipojaa, wavuvi wakaukokota inchi kavu. Halafu wakaikaa kwa kuchagua samaki: wakaweka samaki wazuri ndani ya vyombo na kutupa samaki wabaya.


Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”


Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”


Yakobo na Yoane wana wa Zebedayo waliokuwa wavuvi wenzake na Simoni, walishangaa vilevile. Na Yesu akamwambia Simoni: “Usiogope; tangia sasa utafanya kazi ya kuopoa watu.”


Yeye anakata kila tawi linalokuwa ndani yangu lisilozaa matunda. Naye anasafisha kila tawi linalozaa matunda, kusudi lizae matunda mengi zaidi.


Kama mutu asipokaa ndani yangu, yeye ni kama tawi linalotupwa na kukauka. Matawi yanayokauka yanakusanywa na kutupwa katika moto nayo yanateketea.


Na hata kati yenu kutatokea watu watakaotoa mafundisho ya kupotosha wengine kusudi wawavute waamini kuwafuata.


(Inafaa kuwe matengano kati yenu, kusudi wale wanaokuwa waaminifu wa kweli kati yenu wajulikane.)


Katika safari zangu nyingi nimepata hatari ya mafuriko ya mito, hatari ya wanyanganyi, hatari kutoka kwa wanainchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine. Nilikuwa katika hatari ndani ya miji, katika jangwa, katika bahari na kati ya wandugu za uongo.


ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Sardi hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa na roho zile saba za Mungu na zile nyota saba. Ninajua matendo yako, hakika wewe umekwisha kufa ingawa unajulikana kuwa muzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ