Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 13:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mali iliyofichwa katika shamba moja. Mutu mumoja alipoiona, akaificha tena. Halafu kwa furaha kubwa akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kununua lile shamba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 13:44
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakuna mutu anayejua bei ya hekima, wala hekima haipatikani katika inchi ya wanaokuwa wazima.


Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.


Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Yesu akawaambia mufano mwingine, akisema: “Ufalme wa mbinguni unafanana na mutu mumoja aliyepanda mbegu nzuri ya ngano katika shamba lake.


Alipoona ushanga mumoja muzuri sana, akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kuununua.


“Ufalme wa mbinguni unafanana vilevile na wavuvi wamoja waliotupa wavu ndani ya ziwa, nao ukakusanya samaki wa kila namna.


Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”


Halafu Petro akamwuliza: “Angalia, sisi tumeacha vyote na kukufuata wewe! Basi na sisi tutapata nini?”


Na kila mutu aliyeacha nyumba yake, kaka, dada, baba, mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara nyingi zaidi na kupewa uzima wa milele.


Kwa maana pahali akiba yako inapokuwa, ni pale roho yako inapokuwa vilevile.


Ni vile inavyokuwa, hakuna mumoja wenu atakayeweza kuwa mwanafunzi wangu kama asipoacha vyote anavyokuwa navyo.”


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.


kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ