Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 13:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 13:22
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele, atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako; atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Anayetegemea mali zake ataanguka, lakini mwenye haki atastawi kama jani bichi.


Macho yako yatakapokuwa yanaanza tu kuuona, nao utatoweka mara moja. Maana hakika utajiri unaota mabawa, unaruka na kutoweka katika anga kama tai.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Yawe anawaambia hivi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema: Mulime mashamba yenu mapya; musipande mbegu zenu penye miiba.


Kila mutu anayesema vibaya juu ya Mwana wa Mutu atasamehewa, lakini kila mutu anayesema vibaya juu ya Roho Mutakatifu, hatasamehewa katika ulimwengu huu, wala katika ule unaokuja.


Adui aliyepanda nyasi ni Shetani. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni wamalaika.


Kama vile nyasi zinavyoongolewa kwa kuchomwa katika moto, ndivyo itakavyokuwa vilevile kwa mwisho wa dunia.


Mbegu zingine zikaanguka katikati ya miiba. Ile miiba ikaota na kuzisonga.


Kisha Yesu akawaambia watu wote: “Muangalie, mujilinde na tamaa yote ya mali, kwa sababu mali haiwezi kukinga uzima wa mutu, hata akiwa tajiri sana.”


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi inavyokuwa kwa yule anayejiwekea mali mengi, lakini mbele ya Mungu hahesabiwi kuwa na kitu.”


“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla


Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.


Simoni alipoona kwamba wanafunzi wamepokea Roho Mutakatifu kwa njia ya kuwekewa mikono ya mitume, akaletea Petro na Yoane feza na kuwaambia:


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!


Ingawa vile, mimi ninatangaza mambo ya hekima kwa watu waliokomaa kiroho. Lakini mambo haya si ya hekima ya kidunia, wala ya watawala wa dunia hii watakaoangamizwa.


Hakuna hata mutawala mumoja kati ya watawala wa dunia hii aliyeelewa hekima ile. Kama wangeielewa wasingemutundika Bwana wa utukufu juu ya musalaba.


Mutu yeyote asijidanganye mwenyewe. Kama mutu fulani kati yenu akijizania kuwa mwenye hekima ya kidunia, ajifanye kama mupumbafu kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.


Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Dema amependelea mambo ya dunia hii akaniacha na kwenda Tesalonika. Kreske akaenda Galatia, na Tito akaenda Dalmatia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ