Matayo 13:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja, wanaanguka.
Lakini Yawe anasema hivi: Nitakutendea nini, ee Efuraimu? Nikufanyie nini, ee Yuda? Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi.
Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’
Lakini halizami ndani yao kama mizizi; wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja wanaanguka.
Udongo wenye mawe pahali mbegu zilipoanguka ni mufano wa watu wanaosikia neno na kulipokea kwa furaha, lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanaliaminia kwa muda mufupi tu, nayo majaribu yanapowafikia, wanaliacha.
Wale watu wanaowalazimisha ninyi kutahiriwa, ndio wanaotaka kujionyesha katika mambo yanayoelekea mwili. Lakini wanafanya vile tu kusudi wasiteswe kwa ajili ya kuhubiri habari za musalaba wa Kristo.
Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.