13 Ni kwa sababu hiyo ninasema nao kwa kutumia mifano: kwa kuwa wanaangalia, lakini hawaoni, nao wanasikiliza lakini hawasikii wala hawafahamu.
Watu hao hawajui wala hawaelewi kitu chochote. Wamefungwa macho wasipate kuona na akili wasipate kufahamu.
Musikilize, enyi wajinga na wapumbafu: ninyi munaokuwa na macho, lakini hamwoni, munaokuwa na masikio, lakini hamusikii.
Wewe mwanadamu! Wewe unakaa kati ya watu waasi. Wana macho lakini hawaoni; wana masikio lakini hawasikii.
“Lakini heri kwenu, kwa sababu macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia!
kama vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa migumu, macho yao yasipate kuona na masikio yao yasipate kusikia, na ni hivi wanavyokuwa hata leo.”