Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 13:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa mbinguni, lakini kwao si vile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 13:11
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Yawe amewamwangia roho ya usingizi; macho yenu yasipate kuona enyi manabii, amefunika vichwa vyenu enyi wenye kupata maono.


Basi, kwenu ninyi, maono haya yote ni kama ujumbe ulioandikwa katika kitabu kilichofungwa kwa muhuri. Ukimupelekea mutu yeyote anayejua kusoma, na kumwambia “Unisomee kitabu hiki”, atasema “Siwezi kukisoma kwa sababu kimefungwa kwa muhuri.”


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Wanafunzi wa Yesu wakamwendea na kumwuliza: “Kwa sababu gani unasema na watu hawa ukitumia mifano?”


Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Yesu akawajibu: “Si watu wote wanaoweza kukubali neno hilo munalosema, isipokuwa tu wale wanaojaliwa na Mungu.


Na Yesu akawaambia: “Hakika mutaubeba muzigo nitakaoubeba. Lakini kuikalisha mutu kwa upande wangu wa kuume au wa kushoto si kazi yangu. Ni Mungu peke yake atakayeweka watu aliowatayarisha kwenye nafasi zile.”


Lakini kuikalisha mutu kwa upande wangu wa kuume au wa kushoto si kazi yangu. Ni Mungu peke yake atakayeweka watu aliowatayarisha kwenye nafasi zile.”


Yesu akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini watu wengine wanaokuwa inje ya kikundi chenu wanasikia mambo yote kwa njia ya mifano,


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini kwa watu wengine si vile. Wao wanaambiwa maneno hayo kwa njia ya mifano, kusudi waangalie, lakini wasione kitu, nao wasikie, lakini wasifahamu kitu.”


Yesu akaongeza kusema: “Kwa sababu hii niliwaambia kama hakuna mutu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa anawezeshwa na Baba.”


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Na kati ya wanawake wale kulikuwa mwanamuke mumoja aliyeitwa Ludia, wa muji Tuatera. Yeye alikuwa muchuuzi wa nguo nyekundu za bei kali na mwenye kuogopa Mungu. Mwanamuke yule akatusikiliza kwa maana Bwana alimufungua moyo kusudi apate kufuata kabisa maneno Paulo aliyosema.


Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.


Mungu asifiwe! Yeye yuko na uwezo wa kuwaimarisha katika imani juu ya Habari Njema ninayotangaza kwa kuhubiri ujumbe juu ya Yesu Kristo, kufuatana na ufunuo wa siri iliyofichwa tangia zamani za kale na kale.


Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.


Sasa nitawaambia ninyi siri: sisi wote hatutakufa, lakini sisi wote tutabadilishwa


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Ninatangaza hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichwa kwa watu, na iliyopangwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia kwa ajili ya utukufu wetu.


Kwa hiyo mutuhesabu kama watumishi wa Kristo, wanaoshugulika na ujumbe wa siri wa Mungu.


Ni nani aliyekuweka kuwa mukubwa kuliko wengine? Si Mungu ndiye aliyekupa vitu vyote unavyokuwa navyo? Ikiwa ni hivi, kwa sababu gani unajivuna kama vile haukuvipewa kama zawadi?


Ninaomba Mungu aifungue mioyo yenu ipate kuona mwangaza wake. Kwa hiyo mutapata kujua tumaini munalokuwa nalo kutokana na mwito wa Mungu. Vilevile mupate kujua utajiri mukubwa wa urizi anaouwekea watu wake,


Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.


Ni vigumu sana kuelewa siri hii, lakini ninasema mambo yanayoelekea Kristo na kanisa.


Muniombee vilevile, kusudi Mungu anijalie maneno ya kusema. Kwa hiyo nitaweza kuwajulisha watu kwa uhodari siri ya Habari Njema.


Ninapigana kusudi wapate kuwa na bidii na kuungana katika upendo. Na zaidi ya hii wapate kuwa na uhakika kabisa unaotokana na ufahamu mukamilifu. Hivi wataweza kujua siri ya Mungu, maana yake kumujua Kristo mwenyewe,


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


wanapaswa kushikamana kwa zamiri safi na ukweli wa imani uliofunuliwa.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Lakini munajazwa na Roho Mutakatifu ambaye Kristo alimimia juu yenu, na kwa hiyo ninyi wote munajua ukweli.


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ