“Lakini, ee Mungu kweli utakaa humu katika dunia na wanadamu, ikiwa hata mbingu zenyewe, wala mbingu za mbingu za juu sana hazikutoshi? Namna gani nyumba hii ambayo nimejenga itakutoshelea?
Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?
Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.
Vilevile hamujasoma bado katika kitabu cha Sheria ya Musa kwamba kila siku ya Sabato, makuhani wanaotumika ndani ya hekalu wanavunja Sheria inayoelekea siku ile, nao hawahesabiwi kuwa na kosa?