Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 12:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Yesu akawajibu: “Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu, wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataona kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 12:39
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliikomboa inchi yote iliyokuwa mali ya Israeli, kutokea Pito la Hamati mpaka bahari ya Chumvi. Hivi ndivyo Yawe alivyoahidi kwa njia ya mutumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gati-Heferi.


Lakini Yawe anasema: Mukuje hapa ninyi wana wa wake wachawi; ninyi wazao wa wachawi, wazinzi na makahaba.


Neno la Yawe lilimufikia Yona mwana wa Amitai kusema hivi:


Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataonyeshwa kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.” Kisha Yesu akawaacha na kujiendea.


Yesu akaugua sana kwa huzuni, na kusema: “Sababu gani ninyi watu wa kizazi hiki munataka kuona kitambulisho? Kweli ninawaambia, hamutaonyeshwa kitambulisho!”


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ