Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 12:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 12:34
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi.


Unikinge na shauri baya la waovu, nayo fujo ya watu wabaya.


Wanapiga mutu mukamilifu kwa uficho, wanamupiga kwa rafla bila kuogopa.


Moyo wa mwenye hekima unamwezesha kusema kwa hekima; unayafanya maneno yake yakuwe ya kuvutia.


Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana mule munatokea chemichemi za uzima.


Wapumbafu wanasema maneno ya upumbafu, na mafikiri yao ni kutenda maovu, kutenda mambo ya watu wasiomujua Mungu, kusema maneno ya kumutukana Yawe. Wanawaacha wenye njaa bila chakula, na wenye kiu wanawanyima kinywaji.


Sheria ya Mungu imewekwa pembeni, haki iko mbali; ukweli unakanyagwa katika tribinali, usawa hauwezi kuingia humo.


Hakuna anayemushitaki mwenzake kwa haki, wala anayejitetea kwa ukweli. Munategemea mambo ya bure; munasema uongo. Munafanya mipango ya kuleta hasara na kuzaa uovu.


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


Mutu muzuri anatwaa vitu vizuri toka ndani ya akiba yake nzuri, naye mutu mubaya anatwaa vitu vibaya toka ndani ya akiba yake mbaya.


Lakini vyote vinavyotoka ndani ya kinywa ni vyenye kutoka kwanza ndani ya moyo wake, navyo vinamuchafua mutu.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani mutaweza kuepuka azabu ya jehenamu?


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Halafu watu wengi walimufikia Yoane kusudi awabatize. Naye aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliwaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Mutu muzuri anasema maneno mazuri kutokana na uzuri wa moyo wake. Na mutu mubaya anasema maneno mabaya kutokana na ubaya wa moyo wake. Kwa maana kinywa cha mutu kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo wake.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.


Vilevile kusisikilike maneno ya matusi ya ovyo ovyo wala machafu, kwa maana hayana mafaa. Kinachofaa ni kumushukuru Mungu.


Sisi wote tunakosa kwa njia mbalimbali. Mutu asiyekosa katika masemi yake, huyo ni mutu mukamilifu, naye yuko na uwezo wa kutawala mwili wake wote.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Yawe aamue kati yangu na wewe. Naye ndiye akulipize kisasi lakini mimi sitanyoosha mukono wangu juu yako hata kidogo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ