Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 12:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Na kama Shetani akimufukuza Shetani anajigombanisha yeye mwenyewe, nao ufalme wake utaanguka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 12:26
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Pahali zile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia, ni mufano wa watu wanaosikia habari ya Ufalme na kukosa kuielewa. Na kisha yule mwovu Shetani anakuja na kuondoa mbegu zilizopandwa ndani ya mioyo yao.


Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Lakini Wafarisayo wakasema: “Ni mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”


Sasa ni wakati wa dunia hii kuhukumiwa; sasa mutawala wa dunia hii atashindwa.


Sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa sababu mutawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu,


Na kuelekea hukumu ni kwa sababu mutawala wa dunia hii amekwisha kuhukumiwa.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Malaika wa tano akamwanga kikombe chake juu ya kiti cha kifalme cha yule nyama wa ajabu, na ufalme wake ukafunikwa na giza. Watu wakaanza kutafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu.


Na mufalme wao, ndiye malaika wa lile shimo ndefu la kuzimu, jina lake liliitwa kwa Kiebrania “Abidani” na kwa kigriki “Apolioni” (maana yake “Mwangamizaji”).


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ