Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 12:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Mule ndani mulikuwa mutu mumoja mwenye mukono unaokauka. Nao watu wamoja waliokuwa pale walitafuta sababu ya kumushitaki Yesu; kwa hiyo wakamwuliza: “Sheria yetu inaruhusu kumuponyesha mutu kwa siku ya Sabato?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 12:10
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wapumbafu wanasema maneno ya upumbafu, na mafikiri yao ni kutenda maovu, kutenda mambo ya watu wasiomujua Mungu, kusema maneno ya kumutukana Yawe. Wanawaacha wenye njaa bila chakula, na wenye kiu wanawanyima kinywaji.


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Hakuna anayemushitaki mwenzake kwa haki, wala anayejitetea kwa ukweli. Munategemea mambo ya bure; munasema uongo. Munafanya mipango ya kuleta hasara na kuzaa uovu.


Ole wake muchungaji mupumbafu, ambaye anawaachilia kondoo wake! Upanga uukate mukono wake, na jicho lake la kuume liongolewe! Mukono wake upooze, jicho lake la kuume lipofuke.


Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakamwambia Yesu: “Angalia! Wanafunzi wako wanafanya mambo yanayokatazwa kufanya kwa siku ya Sabato!”


Wafarisayo wamoja wakamufikia kwa kumupima, wakamwuliza: “Sheria yetu inamuruhusu mutu kumufukuza muke wake haizuru kwa sababu gani?”


Watu waliokuwa mule wakamuchunguza Yesu kusudi waone kama atamuponyesha mutu yule kwa siku ya Sabato, wapate sababu ya kumushitaki.


wakimupima kusudi wapate kumunasa katika masemi yake.


Lakini mukubwa wa nyumba ya kuabudia alichukizwa kwa sababu Yesu aliponyesha mutu kwa siku ya Sabato. Kwa hiyo akawaambia watu waliokusanyika pale: “Kuna siku sita za kazi. Basi mufike kwa kuponyeshwa katika siku zile, hapana kwa siku ya Sabato!”


Utuambie basi, Sheria inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana?”


Akawaambia: “Mumeniletea mutu huyu mukisema kwamba anashawishi watu kufanya uasi. Basi nimemwuliza mbele yenu juu ya maneno yale, lakini sikumwona na kosa lolote ninyi munalomushitakia.


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


kwa hiyo Wayuda wakamwambia mutu yule aliyeponyeshwa: “Leo ni siku ya Sabato, na Sheria haikuruhusu kubeba kipoyi chako.”


Wagonjwa wengi walikuwa wakilala katika viingilio vile; kulikuwa vipofu, vilema na wenye kupooza. [Walikuwa wakingoja maji yatikiswe,


Basi, kama munaweza kutahiri mutu kwa siku ya Sabato, kusudi musivunje Sheria ya Musa, kwa nini munanikasirikia kwa sababu nimemuponyesha mutu kabisa kwa siku ya Sabato?


Wao walisema hivi kwa kumupima, kusudi wapate sababu ya kumushitaki. Lakini Yesu akainama na kuandika juu ya udongo kwa kidole chake.


Wafarisayo wamoja wakasema: “Mutu huyu hakutoka kwa Mungu kwa sababu hashiki sheria ya siku ya Sabato.” Lakini wengine wakasema: “Mutu mwenye zambi anaweza kuonyesha kitambulisho kama hiki?” Basi kukatokea mikorogano kati yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ