Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munanyanganya mali za wajane na kuomba maombi marefu kwa kujionyesha. Kwa sababu hii azabu yenu itakuwa kubwa zaidi!]
Na nafasi yoyote watu watakapokataa kuwakaribisha na kuwasikiliza, mutoke kule na mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu. Jambo hili litakuwa ushuhuda juu yao.”