Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 11:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 “Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 11:21
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo ninatubu na kujihukumu; ninajinyenyekeza na kuikaa juu ya mavumbi na majivu.


Nimeyaona machukizo yako: nimeona uzinzi wako na utongozaji wako, na uasherati wako usiousikilia haya, unaoufanya juu ya milima na katika mashamba. Ole kwako wewe Yerusalema! Mpaka wakati gani utabaki bila kutakaswa?


Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.


Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, ninyi mutaazibiwa zaidi kuliko muji wa Tiro na wa Sidona.


Yesu akaondoka pale na kwenda pande za karibu na muji wa Tiro na wa Sidona.


Ole kwa dunia kwa ajili ya vikwazo vinavyokuwa ndani yake! Vikwazo haviwezi kosa kutokea, lakini ole kwa mutu yule anayevileta!


Mwana wa Mutu atakufa sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake, lakini ole kwa mutu yule atakayemutoa! Ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa!”


Yerusalema, Idumea, katika inchi za upande mwengine wa muto Yordani na pande za muji wa Tiro na wa Sidona. Kundi hili kubwa la watu walimufikia Yesu kwa sababu walisikia habari za mambo aliyofanya.


Pale pale Yesu akawalazimisha wanafunzi wake waingie ndani ya chombo na kumutangulia ngambo ingine ya ziwa la Galilaya kuelekea muji Betesaida. Kwa wakati ule alibaki akiaga lile kundi la watu.


Kisha Yesu akaondoka pale, na kwenda katika jimbo lililokuwa karibu na muji Tiro. Akaingia ndani ya nyumba, naye hakutaka mutu ajue kwamba yuko mule, lakini haikuwezekana kwake kujificha.


Kisha Yesu akaondoka kule katika jimbo lililokuwa karibu na Tiro, akapita Sidona na katikati ya inchi ya Miji Kumi, hata akafika kwenye ziwa la Galilaya.


Yesu na wanafunzi wake wakafika Betesaida. Kule wakamuletea Yesu mutu mumoja kipofu na kumwomba amuguse kusudi apate kupona.


Lakini Elia hakutumwa kwa mutu yeyote kati yao, isipokuwa tu kwa yule mujane wa Zarepata, katika inchi ya Sidona.


Yesu akashuka toka kilima pamoja na wanafunzi wake, na kusimama kwenye uwanja. Pale kulikuwa wanafunzi wake pamoja na kundi kubwa sana la watu waliotoka Yerusalema, katika Yudea yote na pande za miji Tiro na Sidona pembeni ya bahari.


Mitume waliporudia toka kuhubiri wakamwelezea Yesu mambo yote waliyofanya. Kisha akaondoka pamoja nao na kwenda kwenye nafasi ya upekee karibu na muji Betesaida.


(Filipo alikuwa muzaliwa wa Betesaida, muji wa Andrea na Petro.)


Basi wakamwendea Filipo wa kijiji cha Betesaida ya Galilaya na kumwambia: “Bwana, tunataka kuonana na Yesu.”


Herode alikuwa amechunga hasira sana juu ya watu wa muji Tiro na wa Sidona. Lakini wakapatana kwa nia moja kwa kumwendea. Kwanza wakasikilizana na Balasto, aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya mufalme. Kisha wakaomba mapatano ya amani kwa mufalme Herode, kwa sababu inchi yao ilitegemea inchi ya mufalme huyo kwa kupata chakula.


Kesho yake tukatua Sidona. Yulio aliyemutendea Paulo mema, akamupa ruhusa ya kwenda kuonana na warafiki zake, wapate kumupa vitu alivyohitaji.


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa sita, kukakuwa tetemeko kubwa la dunia; jua ikageuka kuwa nyeusi kama nguo ya kilio na mwezi ukageuka kuwa mwekundu kama damu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ