Yehu aliporudi kwa wenzake, mumoja wao alimwuliza: “Kuna shida yoyote? Mwenda-wazimu huyu alitaka nini kwako?” Yehu akawajibu: “Si munamujua yeye na namna yake ya kusema?”
Yawe amekufanya wewe Zefania kuwa kuhani kwa pahali pa kuhani Yehoyada, kusudi ukuwe mukubwa wa nyumba ya Yawe. Wewe utashugulika na kumutia katika kifungo na kumufunga kwa minyororo mwenda-wazimu yeyote anayetabiri.
Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.
Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.
Walimu wa Sheria waliotoka Yerusalema, wakasema hivi juu ya Yesu: “Amepatwa na Belzebuli.” Na wengine wao wakasema: “Ni huyo mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”
Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.