Matayo 11:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Huyu ndiye maneno haya yameandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu: ‘Ninamutuma mujumbe wangu akutangulie, kusudi akutengenezee njia utakayopitia!’
Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.
“Kweli ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna mutu anayekuwa mukubwa kuliko Yoane Mubatizaji. Lakini yeyote anayeonekana kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.
Yoane ndiye yule Mungu aliyemutaja kwa njia ya nabii Isaya akisema: “Sauti inatangaza katika jangwa: ‘Mutengeneze njia ya Bwana, munyooshe pahali atakapopita!’ ”