Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.
Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [
“Sheria ya Musa na maandiko ya manabii yalitangazwa mpaka kuja kwa Yoane. Tangu wakati ule, Habari Njema ya Ufalme wa Mungu inahubiriwa, na kila mutu anajiingiza kwa kinguvu ndani ya ufalme ule.
Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”
Wao walichukizwa sana kwa sababu wale mitume wawili walikuwa wakiwafundisha watu na kutangaza kwao kwamba Yesu alifufuka, nao ufufuko wake unahakikisha kwamba wafu watafufuka.