Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Hao ndio wanafunzi kumi na wawili Yesu aliowatuma, akiwaagiza mambo haya: “Musiende katika inchi za watu wa mataifa mengine wala musiingie katika muji wowote wa Samaria.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 10:5
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye akawatuma watumishi wake kwa kuwaita watu wale walioalikwa kwa karamu, lakini hawakutaka kufika.


“Inchi ya Zebuluni na ya Nafutali, kufuata barabara inayokwenda kwenye ziwa, ngambo ya magaribi ya Yordani, katika jimbo la Galilaya, inchi ya watu wa mataifa mengine.


Aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili wawili na kuwapatia uwezo wa kufukuza pepo.


Nyuma ya maneno hayo, Bwana akawachagua watu wengine makumi saba. Naye akawatuma wawili wawili wamutangulie kupita katika kila muji na kila nafasi yeye mwenyewe alipokuwa amekusudia kwenda.


Lakini Musamaria mumoja, alikuwa akisafiri vilevile katika njia ile, akafika kwenye nafasi ile yule mutu alipokuwa. Wakati alipomwona, akamusikilia huruma.


Akainama uso mpaka chini mbele ya Yesu na kumushukuru. Mutu huyo alikuwa Musamaria.


Yesu akawakusanya wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapatia uwezo na mamlaka ya kufukuza pepo, na uwezo wa kuponyesha wagonjwa.


Halafu akawatuma kuhubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwaponyesha wagonjwa,


Kama vile ulivyonituma katika dunia, mimi vilevile nimewatuma katika dunia.


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Babu zetu walimwabudu Mungu juu ya mulima huu, lakini ninyi Wayuda munasema kama Yerusalema ni pahali pa kumwabudia Mungu.”


Akafika karibu na muji mumoja wa Samaria unaoitwa Sikari, uliokuwa karibu na shamba lile Yakobo alilomupa mwana wake Yosefu.


Basi yule mwanamuke Musamaria akamwambia Yesu: “Namna gani wewe Muyuda unaweza kuniomba mimi Musamaria maji ya kunywa?” (Wayuda hawakukuwa na ushirika na Wasamaria.)


Wayuda wakaulizana hivi wao kwa wao: “Mutu huyu atakwenda wapi sisi tusipoweza kumwona? Ataenda kwa Wayuda waliosambazwa kati ya Wagriki na kuwafundisha Wagriki?


Wayuda wakamujibu: “Sisi tulikuwa na haki ya kusema kwamba wewe ni Musamaria na kwamba uko na pepo.”


Lakini mutapokea uwezo wakati Roho Mutakatifu atakaposhuka juu yenu. Nanyi mutakuwa washuhuda wangu katika Yerusalema, katika Yudea yote na Samaria na hata katika inchi zote za dunia.”


Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ