Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 10:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 10:42
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mwanamuke alipokuwa anaondoka, Elia akamwita tena na kumwambia: “Uniletee na kipande cha mukate vilevile.”


Ninakuomba basi tumujengee chumba na kule tumwekee kitanda, meza, kiti na taa, kusudi akitumie kila mara anapotutembelea.”


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Ndivyo hekima itakavyokuwa katika nafsi yako; ukiipata, siku nzuri zitakuja na tumaini lako halitakuwa la bure.


Tupa chakula chako juu ya maji. Nyuma ya siku nyingi utakipata tena!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Ni hivi vilevile Baba yenu anayekuwa mbinguni hataki hata mumoja wa hawa wadogo kupotea.


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Ingekuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kutumbukizwa ndani ya bahari, kuliko kumwangusha mumoja wa wadogo hawa.


Lakini muwapende waadui zenu, muwatendee mema na muwakopeshe pasipo kutumainia kurudishiwa kitu. Halafu mutapewa zawadi kubwa na mutakuwa kweli watoto wa Mungu Mukubwa kwa sababu yeye ni mwema kwa watu waovu wasiokuwa na shukrani.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ