39 Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake, ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu, ataupata tena.
Yule atakayelinda uzima wake, ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake, ataulinda.
Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu ataulinda.
Anayependelea maisha yake atayapoteza, lakini asiyeyashugulikia katika dunia hii, atayachunga hata atakapopata uzima wa milele.
Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.