Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 10:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 10:3
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na kama akikataa kuwasikia watu wale, upeleke habari kwa kanisa. Naye akikataa kusikia kanisa vilevile, umuhesabu kama mupagani na mutenda maovu sawa walipishaji wa kodi.


Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya Yakobo na Yosefu, pamoja na mama ya wana wa Zebedayo.


Yesu alipokuwa akipita, akamwona mutu anayeitwa Matayo, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!” Naye akasimama na kumufuata.


Kulikuwa wanawake wamoja walioangalia kwa mbali. Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya kijana Yakobo na Yose na mwanamuke mwingine Salome.


Kisha alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!” Naye Lawi akasimama na kumufuata.


Andrea na Filipo, Bartolomayo, Matayo, Toma, Yakobo mwana wa Alfayo, Tadeo, Simoni wa kundi la Wazeloti


“Siku moja watu wawili walienda kuomba kwenye hekalu; mumoja alikuwa Mufarisayo na mwingine alikuwa mulipishaji wa kodi.


Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Kule kulikuwa mutu mumoja jina lake Zakayo aliyekuwa mukubwa wa walipishaji wa kodi, naye alikuwa tajiri.


Nyuma ya mambo hayo, Yesu alipoondoka akamwona mulipishaji mumoja wa kodi anayeitwa Lawi, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!”


Natanaeli akamwuliza: “Unanijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Filipo alipokuwa hajakuita, nilikuona wakati ulipokuwa chini ya muti wa matunda ya tini.”


Basi Toma, anayeitwa “Pacha,” akawaambia wanafunzi wenzake: “Nasi tuende vilevile, tukufie pamoja naye.”


Yuda (si yule Yuda Iskariota) akamwuliza: “Bwana, namna gani utajitambulisha mwenyewe kwetu wala si kwa dunia?”


Toma akamwambia: “Bwana, hatujui pahali unapokwenda, basi namna gani tutajua njia?”


Yesu akajibu: “Filipo, nimekwisha kuwa nanyi siku nyingi sasa, nawe haujanijua bado? Aliyeniona mimi amemwona Baba. Basi sababu gani unasema: ‘Utuonyeshe Baba?’


Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Naye akawanyamazisha kwa kunyoosha mukono, kuwaelezea namna Bwana alivyomwondoa katika kifungo. Akawaambia tena: “Muwaelezee Yakobo na wandugu wengine waamini habari hizi.” Kisha Petro akaondoka na kwenda nafasi ingine.


Nao walipomaliza kusema, Yakobo akajibu, akisema: “Wandugu zangu, munisikilize!


Kesho yake tukaenda pamoja na Paulo kwa Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwa kule vilevile.


Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.


Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ