Ni hivi maneno yote mutakayosema katika giza yatasikilika muchana kati. Vilevile maneno yote mutakayosema kwa siri ndani ya chumba chenye kufichama, yatatangazwa juu ya paa la nyumba.
Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini kwa watu wengine si vile. Wao wanaambiwa maneno hayo kwa njia ya mifano, kusudi waangalie, lakini wasione kitu, nao wasikie, lakini wasifahamu kitu.”
Lakini wakati yule Roho wa ukweli atakapokuja, atawaongoza ninyi kufuata ukweli wote kabisa. Yeye hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, lakini atasema tu yale atakayosikia, naye atawatangazia ninyi habari za mambo yatakayokuja.
Alikuwa akibishana na Wayuda katika nyumba ya kuabudia pamoja na watu wa mataifa mengine walioogopa Mungu. Vilevile alibishana kila siku na watu aliowakuta kwenye nafasi ya makutano.
akiwaambia: “Tuliwakataza kwa nguvu musifundishe tena kwa jina la mutu huyu. Na sasa mumeeneza mafundisho yenu katika Yerusalema yote, nanyi munataka kutubebesha lazima ya kifo chake.”