Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 10:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 10:25
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”


Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”


Ninyi munasema kwamba ninafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli. Basi watu wa kikundi chenu wanawafukuza kwa uwezo wa nani? Watu hao wanashuhudia kwa njia ya matendo yao kwamba ninyi ni wakosaji!


Lakini Wafarisayo wakasema: “Ni mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”


Nao wakamujibu: “Tunaweza.” Yesu akaongeza kuwaambia: “Hakika mutakunywa kikombe nitakachokunywa, na kubatizwa kama vile nitakavyobatizwa.


Walimu wa Sheria waliotoka Yerusalema, wakasema hivi juu ya Yesu: “Amepatwa na Belzebuli.” Na wengine wao wakasema: “Ni huyo mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”


Lakini wamoja kati yao wakasema: “Anafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli, yule mukubwa wa pepo.”


Basi ikiwa Shetani akijigombanisha mwenyewe, ufalme wake hautadumu. Ninasema hivi, kwa maana ninyi munasema kama ninafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli.


Tena ikiwa ninafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli, basi watu wa kikundi chenu wanawafukuza kwa uwezo wa nani? Watu hao watashuhudia kwa njia ya matendo yao kwamba ninyi ni wakosaji.


Wengi kati yao wakasema: “Yuko na pepo! Kweli ni mwenda-wazimu! Sababu gani munamusikiliza?”


Watu wale wakajibu: “Wewe uko na pepo. Nani anatafuta kukuua?”


Wayuda wakamujibu: “Sisi tulikuwa na haki ya kusema kwamba wewe ni Musamaria na kwamba uko na pepo.”


Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ